Hakuna asibisha kua mkali Ronaldo ni mkali mara baada ya kudhihisha ukali wake pale baada ya kutangazwa na Uefa kuwa mchezaji bora kwa kuwagaragaza kipa wa Bayern Munich, Manuel Neuer na Arjen Robben.
Mkali huyo aliisaidia sana timu yake ya Real Madrid kutwaa ndoo ya Uefa ametangazwa rasmi kube ndoo hiyo huku akizidi kuliwaza kundi la Uefa msimu huu baada ya kupangwa kundi moja na wakali wa Uingereza majogoo wa jiji Liverpool.
![]() |
Cristano Ronaldo |
Licha ya kutangazwa kua mchezaji bora Ronaldo mwenye umri wa miaka 29 kwa sasa pia aliisaidia timu yake ya Real Madrid kutwaa kombe la Klabu Bingwa Ulaya - Uefa Champions League- msimu uliopita.
![]() |
Ronaldo akiwa na jezi ya Madrid |
Mwanandinga huyo kutoka Ureno alipachika takribani mabao 17 msimu uliopita na kuiwezesha wakali hao wa Hispania kutwaa ndoo hiyo.
Nikimnukuu mwanandinga huyo alisema kuwa alifurahi sana kutwaa tuzo hiyo lakini lazima niwashukuru wachezaji wenzangu kwa sababu bila
timu, tuzo binafsi ni vigumu kuzipata.
![]() |
Ronaldo akiwa ameshika tuzo yake |
Ronaldo aliwazidi Neuer na Robben katika kura zilizopigwa na jopo la waandishi wa habari wapatao 54.
Neuer mwenye umri wa miaka 28, aliisaidia Ujerumani kushinda Kombe la Dunia, huku Robben mwenye umri wa miaka 30, akifunga magoli 21 ya Bayern na matatu kwa timu ya taifa ya Uholanzi iliyofika nusu fainali Brazil.
Ronaldo alifunga mabao matatu - hat-trick - wakati Ureno ilipoichapa Sweden katika mchezo wa kufuzu kucheza Kombe la Dunia, ingawa hakuweza kuwika Brazil, kwani Ureno ilitolewa katika ngazi ya makundi.
Neuer mwenye umri wa miaka 28, aliisaidia Ujerumani kushinda Kombe la Dunia, huku Robben mwenye umri wa miaka 30, akifunga magoli 21 ya Bayern na matatu kwa timu ya taifa ya Uholanzi iliyofika nusu fainali Brazil.
Ronaldo alifunga mabao matatu - hat-trick - wakati Ureno ilipoichapa Sweden katika mchezo wa kufuzu kucheza Kombe la Dunia, ingawa hakuweza kuwika Brazil, kwani Ureno ilitolewa katika ngazi ya makundi.
![]() |
Ronaldo akiwa na jezi ya Ureno |
Lakini kikubwa kilichomsaidia Ronaldo kutwaa tuzi hiyo ni kiwango chake chake katika ngazi ya klabu ambacho kiliweza kushawishi jopo
lililopiga kura, ambalo lilitakiwa kuchagua mshindi kati ya watatu hao
baada ya mchujo kutoka wachezaji 10.
Wakati huo huo Uefa pia ilitangaza viwango vya ubora kwa timu mbali mbali huku Real Madrid ikiongoza,Na hapa nakuletea kumi bora tu ya viwango hivyo:
Timu 10/11 11/12 12/13 13/14 13/15 Points
1.Real Madrid CF | 33.642 | 36.171 | 29.542 | 39.600 | 4.642 | 143.599 | |
2FC Barcelona | 36.642 | 34.171 | 27.542 | 28.600 | 4.642 | 131.599 | |
3.Bayern München | 24.133 | 33.050 | 36.585 | 29.942 | 4.600 | 128.311 | |
4.Chelsea FC | 26.671 | 33.050 | 30.285 | 28.357 | 4.628 | 122.992 | |
5.SL Benfica | 25.760 | 23.366 | 28.350 | 30.983 | 4.550 | 113.009 | |
6.Manchester United | 36.671 | 16.050 | 21.285 | 26.357 | 0.628 | 100.992 | |
7.Atlético de Madrid | 9.642 | 34.171 | 13.542 | 37.600 | 4.642 | 99.599 | |
8.Valencia CF | 21.642 | 25.171 | 22.542 | 26.600 | 0.642 | 96.599 | |
9.FC Schalke 04 | 30.133 | 20.050 | 22.585 | 18.942 | 4.600 | 96.311 | |
10.Arsenal FC | 22.671 | 22.050 | 21.285 | 21.357 | 4.628 | 91.992 | |
No comments:
Post a Comment