Morogoro.Watu wanaodhaniwa kuwa majambazi
walifunga Barabara ya Morogoro - Iringa katika eneo la Njia Panda ya
Kilosa na baadaye kuteka magari na kupora mali za watu.
Tukio hilo lililotokea saa 8:30 usiku wa kuamkia
jana, limekuja siku moja baada ya polisi mkoani hapa, kumtia mbaroni
raia mmoja wa Burundi akiwa na vifaa mbalimbali vinavyotumika katika
utekaji wa magari.
Vifaa hivyo ni pamoja na darubini, mnyororo wenye misumari, visu 10, maturubai na mabomu ya milipuko.
Kwa mujibu wa baadhi ya watu walioshuhudia tukio
hilo, watekaji walikuwa wakirusha mawe na kuvunja vioo vya magari
yaliyokuwa yamefika katika eneo hilo.
Mmoja wa mashuhuda hao ambaye ni dereva wa gazeti
hili, Deo Ngangaa alisema walikuwa wakisafiri kutoka Iringa kuelekea
Morogoro na walipofika jirani na eneo la tukio, walisikia milio ya
risasi na mawe yaliyokuwa yakirushwa.
Alisema walilazimika kujificha hadi milipuko hiyo ilipomalizika ndipo wakaendelea na safari.
Hata hivyo, Dereva huyo alisema walipofika Njia
Panda ya Kilosa, kando ya barabara waliona magogo na mawe huku magari
matatu yakiwa yamepinduka.
Alisema walishuhudia watu kadhaa wakiwa wameanguka
chini akiwamo dereva wa gari lililokuwa likipelekwa Zambia ambaye pia
ni raia wa nchi hiyo aliyejeruhiwa kwa kupigwa pamoja na mjamzito.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Leonard Paul hakupatikana jana
kuzungumzia tukio hilo.
Chanzo Mwananchi.
Chanzo Mwananchi.
No comments:
Post a Comment