Home Traders

Home Traders

Tembelea TK FM Redio 88.5 Tanga

Monday, 1 September 2014

NHC yawakumbuka vijana Muheza

SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC) limekabidhi mashine nne za kufyatulia matofali kwa vijana 40 wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza ili kusaidia wajasiliamali wadogo kupitia vikundi.
Akikabidhi mashine hizo ofisini kwake mwishoni mwa wiki, Meneja wa NHC Mkoa wa Tanga, Isaya Mshamba kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Muheza, Ibrahimu Matovu alisema lengo la shirika hilo ni kuhakikisha wanaisaidia serikali kupambana na wimbi la ukosefu wa ajira kwa vijana.
Alisema mpango uliopo kwa shirika hilo ni kugawa mashine hizo kwa halmashauri zote za jiji la Tanga ambapo halmashauri zaidi ya nne zimekabidhiwa, hivyo mashine hizo zitagawiwa
kulingana na vikundi husika.
Matovu alilishukuru shirika la nyumba kwa jitihada za kupambana na umasikini kwa kuwapa vijana mshine zitakazosaidia kuwapunguzia ukali wa maisha.
Mwenyekiti wa kikundi cha Sarafina kilichopata moja ya mashine hizo, Shafii Ramadhani itawakomboa kiuchumi kwa kuongeza kiwango cha kazi zao.

No comments:

Post a Comment