Mkereketwa
mkuu na mwanachama wa timu ya Simba Mohammed Dewji amesema kuwa angependa kuwekeza Simba ili kubadili mfumo wa
timu hiyo.
![]() |
MO DEWJ |
Akizungumza
na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mo amesema kuwa bajeti ya Yanga na ile ya Azam FC ni mara
mbili ya ile ya Simba, jambo linaloifanya klabu hiyo kuendelea kubaki kuwa
msindikizaji.
Tayari Mo
amesema yuko tayari kutoa Sh bilioni 20 ili kununua hisa asilimia 51 na
kuwekeza ndani ya Simba na atafanya hayo iwapo Simba SC watakubali kumuuzia
asilimia 51 ya hisa kwa Sh. Bilioni 20.
“Nipo tayari kuwekeza
Bilioni 20 kama watanipa nafasi lakini tukubaliane kuwa hakuna mtu atagusa pesa
hizo , tutauza bondi na kwa kila mwaka tutaingiza Bilioni 3.5 na tutatengeneza
mapato ya Bilioni 2 kila mwaka ukijumlisha ni Bilioni 5.5 ambayo itakuwa ni
bajeti ya mwaka,
“Inaniuma sana kuona
klabu imekuja juzi tu leo inatuzidi mafanikio lakini kama Yanga na Azam bajeti
zao kwa mwaka ni Bilioni 2.5 hadi Bilioni 3, sisi tukiwa na bajeti ya Bilioni
5.5 tutakuwa tumewazidi na tutaleta wachezaji wazuri na kocha mzuri,” alisema
na kuongeza.
Aidha Mo amesema kuwa kama akiuziwa asilimia 51 ya hisa na kuwa mmiliki wa
Simba, atawawezesha wanachama wa muda mrefu wa klabu hiyo kupewa hisa bure,
ambazo wataamua wenyewe kuuza, au kununua hisa zaidi.
Mo Pia amesema kuwa mafanikio kwenye mpira, hakuna zaidi ya fedha hivyo Simba haiwezi kuwa na miaka 80 leo haina hata uwanja wa mazoezi hakika inaniuma.
"Mimi ninaamini Simba haiwezi kubadilika kwa kuwekeza kwenye bajeti ya Sh milioni 500 kwa mwaka. Haitawezekana, ndiyo maana nimekuwa nikisisitiza, kwanza Simba inahitaji muwekezaji na si mdhamini.
Mo Pia amesema kuwa mafanikio kwenye mpira, hakuna zaidi ya fedha hivyo Simba haiwezi kuwa na miaka 80 leo haina hata uwanja wa mazoezi hakika inaniuma.
"Mimi ninaamini Simba haiwezi kubadilika kwa kuwekeza kwenye bajeti ya Sh milioni 500 kwa mwaka. Haitawezekana, ndiyo maana nimekuwa nikisisitiza, kwanza Simba inahitaji muwekezaji na si mdhamini.
“Shabaha
yangu ni kuitoa klabu kwenye Bajeti ya Bilioni 1.2 hadi Bilioni 5.5, mashabiki
wa Simba wanahitaji mafanikio ya haraka, lazima tusajili vizuri, tuajiri kocha
mzuri. Ukitenga Bilioni 4 kwa mwaka, tayari umewazidi wapinzani Azam na
Yanga,”.
Amesema lengo lake ni kuifanya Simba itwae ubingwa wa Afrika kwa kushindana na
timu kama TP Mazembe zinazotumia Bajeti ya Sh. Bilioni 20 kwa mwaka.
No comments:
Post a Comment