Home Traders

Home Traders

Tembelea TK FM Redio 88.5 Tanga

Friday, 5 August 2016

Serengeti Boys Kutupa Karata South Kesho

TIMU ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ‘Serengeti Boys’, kesho  itashuka dimbani kumenyana na wenyeji Afrika Kusini katika Uwanja wa Dobsonville ulioko Soweto, kwenye  mchezo wa awali kuwania nafasi ya kufuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, zitakazofanyika Madagascar mwakani.
Kocha mkuu wa Serengeti boys Bakari Shime  amesema kuwa kikosi chake kitaibuka na ushindi kutokana na vijana wake kuyafanyia kazi mafundisho yake anayowapa.
Mchezo huo utakaoanza saa 9.00 alasiri kwa saa za Afrika Kusini wakati huku Tanzania itakuwa ni saa 10.00 jioni katika uwanja ambao hutumiwa na timu ya Moroka Swallows.
 Mchezo huo kwa Serengeti Boys  utakuwa ni mtihani wa kwanza kati ya miwili kabla ya kufuzu kuelekea Madagacar huku mchezo wa kwanza unafanyika Afrika Kusini, kabla ya kurudiana Agosti 21 katika Uwanja wa Azam ulioko Chamazi-nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.


No comments:

Post a Comment