Home Traders

Home Traders

Tembelea TK FM Redio 88.5 Tanga

Tuesday, 26 August 2014

Khalid Rashi aimwaga Chadema na kujiunga na ACT-Tanzania

Katibu wa Wilaya ya Tanga Chadema  Khalid Rashid amejiudhulu wadhifa wake na kujiunga na chama cha Alliance for Change and Transparence (ACT-Tanzania) pamoja na wajumbe tisa wa kamati ya utendaji.Katibu huyo alijivua nyadhifa hizo sambamba kabisa na  Husna Mawe wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha). Wajumbe waliojiuzulu toka chama hicho ni Hussein Baruti, Mohamed Kidege, Hassan Maulid, Juma Yunusi, Zaina Manyeki, Seleman Hassan, Mwanaisha Kambimbaya, Mohamed Sululu na Kisua Mrami Kisua ambaye pia ni mweka hazina.Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jana, Rashid amedai  kuwa sababu za kujitoa zimetokana na kuandikiwa barua ya kusimamishwa uongozi kinyume cha katiba huku akipewa tuhuma kumi zisizo na ukweli.Miongoni mwa tuhuma hizo ni kupingana na maelekezo ya kamati kuu kuhusu kumvua nyadhifa aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe. Sababu nyingine ni namna uongozi taifa ulivyoshughulikia suala lake kishabiki bila kufuata taratibu.

No comments:

Post a Comment