Home Traders

Home Traders

Tembelea TK FM Redio 88.5 Tanga

Wednesday, 27 August 2014

Man United sikio la kufa!!

Bado tunaweza kusema kua Manchester United ni sikio la kufa maraa baada ya hapo jana kupokea kichapo cha mabao 4-0 toka kwa timu ya daraja la kwanza ya MK Dons katika kombe la ligi na kuwatupilia mbali nje ya mashindano hayo.
yawatupa nje ya Kombe la Ligi

United walikiona cha moto kwa kupelekwa kama vile hawakuwepo uwanjani na MK Dons waliokuwa wakicheza mbele ya washabiki 26,969, rekodi ambayo haijapata kuwekwa tangu timu hiyo ianzishwe. 

Will Grigg alianza kucheka na nyavu mara baada ya Jonny Evans  kufanya makosa dakika ya 25 kabla hawajafunga la pili katika dakika ya 63.
Mara baada ya kutinga nyavuni bao la pili,Van Gal alionekana kama amechukia hivi huku akiwataka washabiki wamwamini.
Bao la tatu likiwekwa kimiani na
Benik Afobena kugusa mpira wa kwanza akitokea benchi katika dakika ya 69 la nne   na la pili kwake likiwa la nne kwa jana akatia kimiani kwa kumshinda David de Gea dakika saba kabla ya mpira kumalizika.

1 comment: