Na Kassim Discover
Naaaaaaaaaaaaaaaaaaaam Msomaji wa Tanga Kunani sasa
leo tunakuletea ugonjwa hatari sana wa Ebola ambao unaua na unazidi kuua barani
Afrika na istoshe ugonjwa huu sasa umekua tishio kweli huku Afrika Mashariki
wakijilinda kukabiliana nao ugonjwa huu.
![]() |
Wadudu wa ugonjwa wa Ebola |
Msomaji wa Tanga Kunani hivi unajua ni kwanini
ugonjwa huu uliitwa Ebola?Haya sasa tanga kunani inakupasha kuwa uliitwa ebola
kwasababu uligundulika katika mto Ebola Mnamo mwaka 1976 ambalpo ndipo
ulipopata jina hili,huku wataalamu wakizidi kusema kusema kuwa ugonjwa huu
uligundulika nchi za Sudan na Congo.
![]() |
Mgonjwa mwenye Dalili za Ebola |
Sasa Ugonjwa huu kwa mujibu wa madaktari mbali
mbali umeua pia jamhuri ya Congo huku nchi jirani kama vile ukanda huu wa
Afrika Mashariki wakijaribu kuweka vituo mbali mbali mipakani ili kuzuia
ugonjwa huu kwa wale wagonjwa watakaobanika kuambukizwa ugonjwa huu.
Ikumbukwe
kua si ugonjwa wa hatari wala mchezo kwani hata hao madaktari pia
umewaua,lakini hadi sasa ukikadiriwa kuua zaidi ya asilimia 88 ya watu.
Msomaji
wa Tanga Kunani kwa mujibu wa wataalamu inasadikiwa kua ugonjwa huu
unasababishwa na homa ya ubongo huku ukidaiwa kujulikana kwa mara ya kwanza
mnamo mwaka 1976 katika bara la Afrika,huku watu wapatao takribani 1200 wakisadikiwa kufariki kwa ugonjwa huu wa ebola kati ya 3147.
![]() |
Madaktari wakimpa tiba mwathirika wa Ebola |
Istoshe
msomaji wa Tanga Kunani ugonjwa huu una dalili zake ambazo kwa mjibu wa
madaktari wanasema kua kati ya siki 2 hadi 21 hujitokeza mara baada ya maambukizi lakini zaidi kabisa kati ya siki 8 hadi 10.Hata hivyo dalili hizi kuenda sambamba kabisa na mafua,homa kali,Uchovu wa ndani ya mwili, Misuli
kuuma.Kuumwa kwa Kichwa pamoja na Koo kuvimba.
Hata
hivyo kwa mujibu wa hao hao madaktari ni kuwa mara baada ya mgonjwa kupata
dalili hizo hapo juu,baadae mgonjwa huanza kuharisha,kutapika,upele
mwili,ufanyaji kazi wa figo pamoja na Ini hua ni mdogo sana,inadaiwa pia damu
huvuja ndani ya mwili na hata kutokwa na damu sehemu zote zenye tundu katika
mwil.
Sasa
msomaji wa Tanga Kunani hebu nikupe taarifa fupi tu kuhusu usambaaji wake,ni
kuwa ugonjwa huu usambaaji wake unaweza kusambazwa toka kwa wanyama kama
nyani na hata kwa binadamu kwa kugusa damu ilioathirika au majimaji ama
kidonda.
Naamini sasa Tanga Kunani imekupa ladha na kukuhabarisha kuhusu ugonjwa huu hatari wa Ebola,tukutane siku nyengine katika makala nyengine.
Naamini sasa Tanga Kunani imekupa ladha na kukuhabarisha kuhusu ugonjwa huu hatari wa Ebola,tukutane siku nyengine katika makala nyengine.
No comments:
Post a Comment