Home Traders

Home Traders

Tembelea TK FM Redio 88.5 Tanga

Saturday, 13 September 2014

Nchi 10 za kiarabu kuisaidia Marekani

Waziri wa maswala ya kigeni nchini Marekani John Kerry amepinga ripoti kwamba mataifa ya kiarabu hayaungi mkono moja kwa moja juhudi zake za kubuni muungano wa kukabiliana na kundi la wapiganaji wa himaya ya kiislamu.
John Kerry nchini Uturuki
Akizungumza nchini Uturuki katika ziara ya eneo la mashariki ya kati,amesema kuwa ameridhishwa na majibu aliyopata kutoka Saudi Arabia na mataifa mengine.
Lakini amesema kuwa si sahihi kwa Iran kujiunga na juhudi za kimataifa dhidi ya wapiganaji hao.
Bwana Kerry anatarajiwa kuelekea nchini Misri hii leo.
Mataifa kumi ya kiarabu yamekubali kuisaidia marekakani.
Chanzo BBC

No comments:

Post a Comment