Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imezindua rasmi sarafu mpya ya Sh500 itakayoanza kuingia katika mzunguko wake Oktoba mwaka huu.
![]() |
Muonelano wa Sarafu mpya |
Kwa mujibu wa mkurugenzi wa huduma za kibenki wa BoT, Emmanuel Boaz alisema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Daressalaam na kusema kuwa Serikali
imefanya uamuzi huo ili kurahisisha upatikanaji wa chenji na kutunza
ubora wa fedha.
“Noti ya Sh500 ndiyo inayopitia mikononi mwa
wananchi wengi hivyo kuchakaa mapema. Lakini kutokana na gharama ya
kuzichapisha ukilinganisha na sarafu ambazo hudumu kwa muda mrefu,
tumeamua kuziondoa noti na kuleta sarafu yenye thamani ile ile.
Aliendelea kusema kua Kuna taratibu zinaendelea kukamilishwa kabla
hazijaingizwa katika mzunguko mnamo mwezi wa kumi mwaka huu.
Aidha Bwana Emmanuel ameendelea kusema kua sarafu hizo zitakapoanza kutumika hakutakuwa na haja ya wananchi kwenda kubadilisha noti walizonazo kwani zitakuwa zinatumika pamoja hadi zitakapopotea katika mzunguko.
Aidha Bwana Emmanuel ameendelea kusema kua sarafu hizo zitakapoanza kutumika hakutakuwa na haja ya wananchi kwenda kubadilisha noti walizonazo kwani zitakuwa zinatumika pamoja hadi zitakapopotea katika mzunguko.
Sarafu hiyo ina umbo la duara, lenye kipenyo cha
milimita 27.5 na michirizi pembeni ikiwa na uzito wa gramu 9.5. Mbele
ina picha ya Rais wa kwanza wa Zanzibar, Sheikh Abeid Aman Karume na
nyuma ni nyati.
Pesa hiyo ya Shillingi Mia Tano iliwahi kupitia katika hatua mbali mbali tazama hapo chini kama zinavyoonekana ya picha zake.
Pesa hiyo ya Shillingi Mia Tano iliwahi kupitia katika hatua mbali mbali tazama hapo chini kama zinavyoonekana ya picha zake.
No comments:
Post a Comment