Home Traders

Home Traders

Tembelea TK FM Redio 88.5 Tanga

Sunday, 28 June 2015

Mizengo kayanza Peter Pinda apata wadhamini 1435

Katika harakati za kusaka nafasi ya kutaka kuteuliwa na chama chake kwa ajili  ya kupewa ridhaa ya kugombea urasi na kuwa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mheshimiwa waziri Mkuu  Mizengo kayanza Peter Pinda hatimae siku ya leo alikuwepo  hapa Tanga mchana katika ofisi za ccm  mkoa na kujipatia jumla ya wadhamini 1435 waliojitokeza kumdhamini.
Picha na Miktaba
Pinda akizungumza na wanachama wa chama hicho katika ofisi za chama hicho zilizopo Barabara ya 21  amesema   kuwa katika watu 41 waliojitokeza kuomba ridhaa katika chama chao,amesema kuwa    mgombea yoyote  atakaechaguliwa atamuunga mkono huku akiwaomba pia wanachama wa chama hicho   wamuunge mkono atakaechaguliwa  na  ambao pia hawatabahatika kuchaguliwa  wasinung’unike.


Pia amempongeza   Mbunge viti maalum wa ccm Ummy Mwalimu kuwa ni jembe linalofanya kazi yake kisawa sawa huku akiwaasa wanawake kuwa wamtumie vizuri basi wanaweza kufika mbali zaidi.


Na hata hivyo amewashukuru sana wana Tanga kwa  mapokezi  yao kwake.

No comments:

Post a Comment