Home Traders

Home Traders

Tembelea TK FM Redio 88.5 Tanga

Thursday, 28 July 2016

Wiki ya Simba Day Yazinduliwa

Katika kuadhimisha miaka 80 tangu Simba ianzishwe, klabu  ya wekundu wa msimbazi Simba  imeamua kusherekea siku hiyo kwa kuialika  timu ya Inter Club ya Angola  katika tamasha la (Simba Day)
Rais wa Simba Evans Aveva akizungumza na waandishi wa habari leo

Hata hivyo Uongozi wa  hiyo umepanga maadhimisho hayo kuzinduliwa na mkutano mkuu wa wanachama utakaofanyika katika bwalo la maofisa wa Polisi Oysterbay Jumapili Julai 31.

Akuzungumza na waandishi wa habari leo Rais wa Simba, Evans Aveva amesema  kuwa watawashangaza mashabiki wao kwa ‘suprise’ kubwa ya wachezaji waliowasajili msimu huu kwani kuna wachezaji ambao watatangazwa na kuwashangaza mashabiki wetu.

Kikosi hicho cha Inter Club kitapambana na Simba katika mchezo wa tamasha la Siku ya Simba ambayo litafanyika Agosti 8, siku ambayo Simba itakua inatimiza miaka 80 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1936.

Inter Club inanolewa na kocha wa zamani wa Simba, Zdravko Logarusic ambaye ameinoa Simba msimu wa 2014/15 kabla ya kutupiwa virago baada ya kufungwa mabao 3-0 na Zesco United katika tamasha la siku ya Simba.

Wakati huo huo Viongozi na wanachama mbalimbali wa Simba watachangia damu katika hospitali mbalimbali ikiwa ni kuungana na jamii.

No comments:

Post a Comment