Home Traders

Home Traders

Tembelea TK FM Redio 88.5 Tanga

Thursday, 28 July 2016

Mtoto ageuka kuwa Mlezi Korogwe

MWANAFUNZI wa kike anayesoma darasa la sita katika shule ya msingi Zumnati  iliyopo Wilayani Korogwe Mkoani Tanga amegeuka mlezi baada ya mama yake kumtoroka mara kadhaa na kumtelekezea wadogo zake wawili  huku mmoja kati yao akiwa ni mlemavu wa viungo.

TK FM imetembelea nyumbani kwa msichana anayeishi katika kata ya masugulu wilayani humo  anayefahamika kwa jina la HELENA THOMAS  na kuzungumza naye, ambapo amesema kuwa mama yake huwa na tabia ya kuondoka zaidi ya wiki mbili kwa kisingizio kuwa anatafuta pesa za chakula.
Aidha FELISTA ISSA ambaye ni mwalimu wa mwanafunzi huyo amesema kuwa kitendo kinachofanywa na mama huyo kimemfanya Helena kutokuwa na maendeleo mazuri darasani kutokana na majukumu aliyonayo na kuwataka wakinamama kutokwepa majukumu ya familia.
Hata hivyo  TK FM imezungumza na mtendaji kata  MUSSA TWAHA ambaye amekiri kuwafahamu watoto hao na kusema kuwa  jitihada za kumsaka mama huyo aliyekosa huruma zikiendelea  kwa ajili ya kumfikisha katika vyombo vya sheria.

No comments:

Post a Comment