Kinda jipya la Azam Enock Atta Agney |
Aidha
Atta amesea kuwa amefurahi sana kuwa Azam fc
na amekuja kushinda makombe pamoja na kuweka historia ndani ya timu hiyo kabla hata hajaondoka huku akisema kuwa amejiandaa
kuzikabili changamoto zote zilizopo
mbele yake .
Tayari
nyota huyo ameshasaini mkataba wa miaka miwili kuwatumikia mabingwa hao akipewa
jezi namba 10, ambapo jana aliweza kuanza rasmi mazoezi na wachezaji wenzake
huku akionekana kuwafurahisha zaidi makocha kwenye mazoezi hayo
Hata hivyo
kuhusiana na utofauti kati ya Tanzania na Ghana amesema kuwa moja ya utofauti mkubwa wa soka la Tanzania
na Ghana ni namna ya uchezaji, Ghana wakicheza soka la kumiliki mpira na nguvu
tofauti na Tanzania huku akidai kuwa aina yao ya uchezaji ndio iliyofanya
wakapata matokeo bora dhidi ya Yanga.
“Ni
vizuri kwangu kuwa hapa, bado sijalijua sana soka la hapa, najua soka la Ghana
lipo juu kuliko hapa, lakini unapokuwa mchezaji unahitaji kubadilisha
mazingira, unatakiwa kuhama timu bila kujali nini kitatokea na cha muhimu ni
kupambana wewe mwenyewe kwa kufanya kazi kwa bidii,” alisema.
Mipango
yake ya baadae kwa mchezajji huyo kucheza
Ulaya, lakini amedai kuwa si lazima sana
kucheza huko ili afanikiwe bali hata Afrika
panatosha na kumfanya mtu kuwa na maisha bora cha msingi ni yeye kufanya kazi
kwa bidii.
“Kila
mchezaji anaheshimu kucheza soka Ulaya, hii ni kutokana unapocheza Ulaya
unaweza kutatua matatizo yako mengi kwenye maisha, hayo ni kwa mujibu wa maneno
ya watu, lakini mimi naamini ya kuwa popote panaweza kuwa Ulaya inategemeana na
wewe unaifanyaje kazi yako.
No comments:
Post a Comment