MFANYABIASHARA
Mohamed Gulam Dewji ametoa mfano wa hundi Sh. Milioni 100 kama mchango wake
katika usajili wa klabu hiyo kuelekea msimu ujao.
Mo Dewji ametoa mfano wa hundi hiyo leo ofisini kwake, Jijini Dar es Salaam
akimkabidhi Rais wa Simba SC, Evans Aveva.
Kufuatia
mchango huo wa Dewj AVEVA amemshukuru Dewj kwa msaada huo huku akisema kuwa bado
timu inahitaji Sh. Milioni 320 kukamilisha
usajili, ingawa hakusema bajeti nzima ya usajili ya klabu hiyo ni kiasi gani.
“Ninashukuru sana kwa msadaa huu kutoka kwa mwanachama wetu, na sasa
ninashukuru tunaweza kumsajili Frederick Blagnon kutoka Ivory Coast,”alisema
Aveva.
Na wakati akipokea mfano wa hundi
hiyo leo, Aveva alisema ameyakubali mabadiliko kwa moyo mmoja na atayasimamia
kuhakikisha yanakwenda haraka ili kutimiza azma ya Simba kuwa ya kutisha siyo
tu Tanzania, bali Afrika nzima.
Pamoja na hayo, Aveva akawataka wanachama zaidi wa Simba kuchangia sehemu iliyobaki, Sh. Milioni 320 katika bajeti ya usajili ya klabu.
Pamoja na hayo, Aveva akawataka wanachama zaidi wa Simba kuchangia sehemu iliyobaki, Sh. Milioni 320 katika bajeti ya usajili ya klabu.

No comments:
Post a Comment