Muargentina Angel di Maria hatimae anakaribia kutua Manchester United na kunachosubiriwa muda wowote toka sasa ni vipimo vya afya kwa amchezaji huyo na kuanza rasmi kibarua chake na mashetani hao wekundu wa Manchester ambao imeanza vibaya mchezo wake wa kwanza baada ya kula kichapo katika mchezo wake wa kwanza kabla mchezo wake wa pili kutoka sare na wakali paka weusi, sasa ni dhahiri shahiri Van Gall amevunja benk na kumchomoa Mchezaji huyo toka Reala Madrid.
De Maria alitarajia kwenda nchini Uingereza mchana huu kwa vipimo lakini wataalamu wa kabumbu wanaamini kua huu utakuwa ni uhamisho mkubwa na kuivunja rekodi iliyokuwa imewekwa misimu kama mitatu iliyopita na Fernando Tores toka Liverpool kuelekea Chelsea kwa da ya uhamisho wa £50m.
Manchester United imekubaliana na pande zote mbili na kuweka kiasi cha £63.9m ambayo hii tunaweza kuiita rekodi ya kiingereza.
Karibu sana Old Traford
ReplyDelete