Home Traders

Home Traders

Tembelea TK FM Redio 88.5 Tanga

Monday, 25 August 2014

Sony yaufunga mtandao wa Play Station

Kampuni ya Sony hatimae umeufunga Mtandao wa Sony Playstation   kufuatia  hofu ya kushambuliwa kwa  mtandao wake wa kutoa huduma ya playstation.

Katika ujumbe kwenye mtandao wake , Sony imesema kuwa hakuna habari za watu binafsi zilizohatarishwa kufuatia shambulizi hilo.
Siku ya jana "Jumapili"ndege aliyokuwa akisafiria mmojawapo wa maafisa wakuu wa Sony, ililazimika kubadilisha mkondo kufuatia hofu ya kulipuliwa.
Baadaye ilibainika kuwa kundi linalodai kutekeleza shambulizi hilo la mtandao, kupitia kwa mtandao wa kijamii wa Twitter uliashiria kuwepo kwa tishio la usalama kwa ndege hiyo.
 Katika taarifa hiyo Sony ilisema kuwa “mtandao wa Playstation na mtandao wa burudani wa Sony iliathirika kufuatia jaribio la kufululizia tovuti zao watumiaji wengi na kuizuia kutoa huduma hata hivyo kampuni hiyo imesema kuwa  itajitahidi kusuluhisha swala hili na wanaamini kuwa  kuwa hali  ya huduma zake itarejea   haraka iwezekanavyo.
Hata hivyo Sony imesema kuwa wapelelezi wa FBI wanachunguza tishio la usalama kwa ndege aliyokuwa akisafiria rais wa Burudani ya Sony Mtandaoni John Smedley, ambayo ilitarajiwa kutua San Diego lakini ikalazimika kubadilisha mkondo na kutua Phoenix, Arizona.
Mtandao huo wa sony wenye zaidi ya wateja milioni 52 wa Sony Playstation umewahi kushambuliwa na wavamizi wa mtandaoni hapo awali, likiwemo shambulizi lililoiba habari za siri za mtandao huo, mwaka 2011.
Hii leo Sony inatarajiwa kurekebisha usalama wa mtandao huo ambao hufanyika mara kwa mara kwa mtandao wake wa PlayStation.
Baada ya 1740 BST, huduma fulani zikiwemo duka la PlayStation, akaunti ya usimamizi na usajili ya PSN, huduma za burudani na michezo ya mtandaoni hazitakuwepo, kwa sababu ya marekebisho.

No comments:

Post a Comment