Home Traders

Home Traders

Tembelea TK FM Redio 88.5 Tanga

Monday, 25 August 2014

Vijue vituo 3 vya Afya kwa Ajili Ya Kudhibiti Ebola

Ugonjwa w Ebola hakuna asieusikia jinsi unavyotesa wanadamu na kuua kwa dakika chache sana,kufuatia hayo sasa Serikali ya Tanga ulitenga vituo vikuu vitatu vya Afya  ikiwa ni hatua ya maandalizi ya kudhibiti watu wataobainika kuambukizwa virusi vya homa hiyo ya Ebola
Tukiwa kama Tanga Kunani leo hii ni bora mkazi wa Tanga uvifahamu vituo hivyo kwa manufaa yetu kwa pamoja,Mkuu wa mkoa wa Tanga Chiku Gallawa aliwahi kubainisha siku chache zilizopita kuwa vituo hivyo ni kile  cha mpaka wa Horohoro wilayani Mkinga, Masiwani Shamba na Maramba.
Alisema kuwa timu maalumu ya mkoa ya wataalamu wa afya, tayari inakagua uwezo wa vituo vingine vilivyotengwa na halmashauri nyingine za mkoa huo, kama vinastahili kupokea wagonjwa wa aina hiyo.
Alisema ingawa mpaka sasa hakuna mgonjwa wa ebola nchini, serikali imechukua hadhari hiyo, kuwaondoa wasiwasi wananchi kutokana na mwingiliano wa wageni kutoka nchi jirani kupitia mpaka wa Horohoro.
Alisema vituo hivyo vitatu vimeimarishwa kwa kupelekewa vifaa tiba, madaktari na wauguzi wenye stadi za kutosha na vitatumika kutoa huduma kwa wagonjwa watakaobainika.

No comments:

Post a Comment