Home Traders

Home Traders

Tembelea TK FM Redio 88.5 Tanga

Monday, 25 August 2014

waliofariki ajali ya Bomu sasa wafikia watu wanne

Bomu linalodhaniwa kutupwa kwa mkono na majambazi kutoka nchi jirani ya Burundi hatimae sasa limesababisha watu takribani wanne kufariki dunia hadi sasa,majeruhi  Regina Mzakule (66) amefariki dunia na kufanya idadi ya waliokufa katika tukio la bomu la kutupa kwa mkono ndani ya gari la abiria wilayani Buhigwe, Kigoma kufikia wanne.
Kwa mujibu wa  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Joshua Monge alisema alipokea majeruhi saba wa tukio hilo akiwemo marehemu huyo.
Alisema marehemu huyo alipata majeraha makubwa na vipande vya chuma kumuingia tumboni.
Aliwataja majeruhi watatu walioruhusiwa kuwa ni Honolina Benjamini (42), Kabula Matius (40) na Agripina Jeremia (45) wakati wanaoendelea na matibabu ni Shukrani David (32), Tedy Charles (25) na Osward Samweli.

No comments:

Post a Comment