Home Traders

Home Traders

Tembelea TK FM Redio 88.5 Tanga

Saturday, 8 November 2014

Mgambo yapoteza mbele ya Yanga

Young Africans imebuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya timu ya JKT Mgambo ya jijini Tanga mchezo uliofanyika jioni ya leokatika  dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, huku Saimon Msuva akibuka shujaa kwa kukwamisha wavuni mabao yote mawili.

Young Africans iliuanza mchezo kwa kasi kwa lengo la kusaka mabao ya mapema, lakini kutokua makini kwa washambuliaji wake Jaja, Coutinho na Ngasa kulipelekea kukosa mabao ya wazi dakika 45 za kipindi cha kwanza na kufanya timu kwenda mapumziko zikiwa 0-0.
Kipindi cha pili Young African illifanya mabadiliko kwa kuwatoa Haruna Niyonzima na Geilson Santos "Jaja" na nafasi kuchukuliwa na Saimob Msuva na Jerson Tegete ambao waliongeza kasi ya mchezo na mashambulizi langoni mwa Mgambo JKT.
Dakika ya 74 ya mchezo, Saimo Msuva aliipatia Young Africans bao la kwanza baada ya kuitendea vyema pasi ndefu ya kiungo Mbuyu Twite aliyompenyezea na kumkuta mfungaji ambaye aliudokoa mpira huo na kujaa wavuni na kumuacha mlinda mlango wa Mgambo JKT Said Lubawa akigaa bila ya kujua cha kufanya.
Baada ya bao Mgambo JKT walicharuka na kufanya mashambulizi kadhaa langoni kwa Young Africans kwa lengo la kusaka bao la kusawazisha, lakini mashambulizi yao yalikuta yakiokolewa na na walinzi wa Young Africans pamoja na mlianda mlango Deo Munish "Dida"
Huku baadhi ya washabiki wakianza kutoka nje wakijua mchezo umemalizika kwa ushindi wa bao 1, Saimon Msuva tena aliipatia timu yake ya Young Africans bao la pili baada ya pasi aliyotanguliziwa na kiungo Hassan Dilunga kuitumia vyema na kuachikia shuti lililojaa wavuni moja kwa moja.
Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizka, Young Africans 2 - 0 Mgambo JKT.
Kwa ushindi wa leo Young Africans inakamata nafasi ya tatu nyuma ya Azam FC iliyoko nafasi ya pili huku wakiwa sawa kwa kwa point na mabao ya kufunga na kufungwa, Mtibwa Sugar wakiendelea kushika nafasi ya kwanza.

No comments:

Post a Comment