Katika muendelezo wa ligi kuu bara hapo kesho ni bonge la mechi pale Chamanzi amapo timu ya nyumbani Coastal watakapokuwa wageni wa Azam fc pale Chamnznzi Mbande.
Akizungumza na TK msemaji wa Coastal Union Oscer Asenga amesema kuwa kuanzia maandalizi yamekamilika kwa asilimia 95.
Asenga amesema kuwa wanaingia katika mchezo huo wakiwa na malengo makubwa kuhakikisha wanapata matokeo mazuri ili kuwahikikshia kukamata usukani wa ligi kuu bara.
Coastal bado wana historia mbaya na dimba la Chamanzi hivyo kesho wanatakiwa kuwapa matumaini makubwa kwa wana Tanga kwa kushinda mchezo huo.
Nae jemedari Said akizungumzia mchezo wa kesho amesema kuwa wapo vizuri na wamejiandaa vizuri kwa mchezo huo wa kesho licha ya mchezo huo kua mgumu sana hapo kesho.
No comments:
Post a Comment