akiidhinisha mafanikio yaliyopatika katika kipindi kizima cha miaka mitano yake lakini pia akizitaja changamoto kubwa zilizokuwa zikiikabili halmashauri ya Muheza.
Mwenyekiti wa Halamashauri ya Muheza Amiri Kiroboto Kushoto (Picha Maktaba) |
Akizungumza katika kipindi cha AMKA NA TK kinachorushwa na kituo cha 88.5 TK FM Mheshimiwa
Kiroboto amesema kuwa baraza hilo limevunjwa kwa mujibu wa maelekezo toka TAMISEMI kwa madiwani na mabaraza yao
yote yavunjwe siku hiyo.
Kiroboto
amesema kuwa changamoto nyingi sana
amekutana nazo kutokana na kuwa na madiwani takribani 46 huku kila mtu akiwa na fikra zake lakini
kikubwa walikabiliana nazo kwani tangu waanze mwaka 2010 hadi sasa wapo salama
na hakuna hata ugomvi uliojitokeza katika baraza lake wala mgomo.
Lakni
changamoto kubwa amezitaja kuwa ni katika miradi ya maendeleo huku asilimia
kubwa ikifikiwa katika suala zima la utekelezaji wa Maji.
Wakati huo huo Kiroboto amesema kuwa hayupo tayari tena
kugombea katika nafasi yoyote ile ya juu
ya Uongozi na sasa inatosha ilobaki ni kuwachia wengine ili waweze kuongoza.
Mheshimiwa Kiroboto amewashukuru sana wakazi wa muheza na kuwaacha na neno la kuondokea kwa kuwaambia kuwa anawapenda sana wana Muheza "Muheza ni Kwangu na wana Muheza ni wangu" akamaliza kusema kuwa kuwa
huwezi kuitwa jemedari kama
hukuishinda mitihani hivyo anashukuru anaondoka madarakani akiiacha Muheza ikiwa salama.
No comments:
Post a Comment