Home Traders

Home Traders

Tembelea TK FM Redio 88.5 Tanga

Thursday, 9 July 2015

Watanzania watakiwa kutochagua Wala Rushwa

Watanzania wametakiwa kuhakisha kuwa katika kipindi hiki ambacho taifa linafanya uchaguzi mkuu wanahakikisha kuwa hawawachagui viongozi ambao wana aina yoyote ya doa la rushwa na wenye uchu wa madaraka kwani kwa kufanya hivyo kuna uwezekano mkubwa wa nchi kuingia katika machafuko makubwa kwani watu hao watakapoingia madarakani wataendesha nchi kwa manufaa ya kikundi kidogo cha mafisadi ambacho kitakuwa kikiwazunguka.

Hayo yamesemwa na washiriki wa mdahalo maalum lililoandaliwa na taasisi ya Mwalimu Nyerere lenye maudhuhi ya amani na umoja hasa katika kipindi hiki ambacho taifa linaelekea katika uchaguzi mkuu huku  mkurugenzi wa taasisi iliyoanda kongamano hilo mzee Joseph Butiku akisema katika mchakato unaoendelea sasa katika chama cha mapinduzi na taifa kwa ujumla yapo mengi yameanza kufanyika kinyume na utaratibu.
 
Naye aliyekuwa mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya katiba mzee Josesph Warioba amesema ni lazim taifa lirudi katika hadhia yake ya awali na siyo kila mtu kijifanyia ambo kama anavyotaka kama vile hakuna utawala wa sheria.
 
Profesa Mwesigwa Baregu katika mdahalo huo amesema nchi inaingia katika uchaguzi ikiwa inaombwe la katiba jambo ambalo kama nchi haitakuwa makini yatatokea mambo kama yaliyotokea huko Kenya ambapo watu walpoteza maisha kwani nao walikuwa kwenye uchahuzi kama ilivyo Tanzania kwa sasa.
 
Jaji mstaafuAamiri Manento na amabye alikuwa mwenyekiti wa tume ya haki za binadamu akitoa mada amesema matatizo mengi yanaletwa na   serikali tena kupitia vyombo vyake vya dola kama polisi na hivyo inapaswa kujiangalia upya .
 
Katika hatua nyingine mwanaharakaati na aliyewahi kuwa mjumbe wa tume ya mabadilko ya katiba bw haumprey polepole ameutaka ukawa kuacha ubinafsi na  huku ccm akitaka kuhakisha katika mkutano wao  unaeendelea dodoma kuhakisha wanatoa jina la mtu safi ili kulinusuru taifa huku rais  chama cha  wanasheria  wa zanzibar  akisema sheria zipo ili zilete haki na siyo kukandamiza haki za watu.

No comments:

Post a Comment