Home Traders

Home Traders

Tembelea TK FM Redio 88.5 Tanga

Thursday, 9 July 2015

Tani zaidi ya Elfu 20 za shehena ya mafuta Yaanza Kushushwa Tanga

Tani zaidi ya Elfu 20 za shehena ya mafuta aina ya Petrol na Diesel zimeshushwa katika bandari ya Tanga tayari kuanza kusambazwa kwa wafanyabishara mbalimbali nchini ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la serikali la kutumia bohari kuu ya mafuta iliyopo jijini Tanga kwa ajili ya kupunguza msongamano uliopo jijini Dar es Salaam.

Walizungumz na waandishi w habari hapo jana mara baada ya 
  meli ya mafuta ya kampuni ya ''Ardmore Sea Marine''   kuanza zoezi la kushusha shehena ya mafuta, mkurugenzi mkuu wa huduma za nishati na madini nchini Bwana Felix Ngamilagos amesema kuwa mwanzon wa mwaka huu timu ya wataalamu ianze kazi kwa ajili ya kuanza kutumika kwa bandari ya Tanga kuanza kazi mara moja.
 Hata hivyo amesema kuwa  mpango huo ni mkakati wa serikali wa kuhakikisha kuwa foleni za magari makubwa kutoka mikoa mbalimbali zinapungua ambazo pia zitasaidia kupunguza uharibifu wa mazingira na miundo mbinu ya barabara.
 Awali Katika kikao cha pamoja kilichoshirikisha wafanyabiashara wa magari, viongozi wa dini, na kijamii, baadhi ya wajumbe wa kikao hicho wameiomba serikali kutilia mkazo zoezi la ushushaji wa mafuta kwa ajili ya uchumi wa serikali na wananchi wake kwa sababu kulikuwa hakuna sababu ya serikali kuacha kutumia bandari ya Tanga yenye miundo mbinu ya kutosha kupitishia shehena zake ambazo ndio nguzo kuu za kukuza uchumi nchini.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Tanga akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mheshimiwa Said Magalula ametoa mchanganuo kuhusu tani elfu 2o za Mafuta hayo.
Kufuatia hatua hiyo  muwakilishi wa mafuta inginia Michael Mjinja ametoa ufafanuzi kuhusu wakazi wa Tanga na fursa hiyo  huku reli ya Tanga ikichukua nafasi yake na kurudi kama ilivyo awali huku wafanyabishara na wananchi kwa ujumla kuchangamnkia fursa hiyo katika zoezi la kukuza uchumi wao ili mkoa wa Tanga uweze kukuza pato la taifa na mtu mmoja mmoja.

No comments:

Post a Comment