Home Traders

Home Traders

Tembelea TK FM Redio 88.5 Tanga

Wednesday, 15 July 2015

MAHUJAJI ZAIDI YA 27 WAMEUAWA.Na RAMADHANI MAKERO


Mahujaji zaidi ya 27 wameuawa kufuatia mkurupuko uliotokea katika warsha moja ya kidini katika jimbo la Andhra Pradesh nchini India 

Mkanyagano huo wakati wa kuanza kwa sherehe za Maha Pushkararu ambapo maelfu ya watu waliokuwa wamekusanyika kuoga kwenye maji ya mto Godavari walianza kusukumana 

Mkurukupo huo ulitokea majira ya saa nane na nusu katika mji wa Rajahmundry,polisi wasema kuwa umati ulikimbia kwenda kwa lango la kuingia mtoni.

Mkurupuko kama hii hutokea kwa wingi wakati wa Warsha za kidini nchini India ambapo watu wengi hung'ang'ania nafasi moja katika maeneo madogo 

Mahujaji hao wa dini hiyo wanaamini kuwa kuoga maji ya mto huosha mtu madhambi yake.

"Inahuzunisha mno kuwa mahujaji walikuwa wakitarajia kuosha madhambi yao wanaangamia"alisema Waziri mkuu wa jimbo hilo la Andhra Pradesh bwana Chandrababu Naidu,

Mwaka wa 2013 watu 115 walipoteza maisha yao katika mkurupuko uliotokea katika hafla ya kidini ya Wahindu katika jimbo la Madhya Pradesh.

No comments:

Post a Comment