chama cha wananchi CUF hatimae umekamilika kwa asilimia kubwa huku kata takribani tano zikisalia lakini zikiwa zipo katika hatua ya mwisho ambazo kata hizo ni Magaoni,central,nguvumali,maweni na masiwani shamba
Akizungumza na AMKA NA TK Diwani wa kata ya
Mwanzange CUF Mheshimia Rashid Jumbe amesema kuwa takribani wagombea wengi waliopitishwa ni wale wale isipokuwa
kata ya Marungu ambae aliyekuwa Diwani wa kata hiyo Mheshiwa Mohamed Mambeya amejiunga na chama cha Mapinduzi CCM huku kata ya
Tongoni aliyekuwa Diwani wa kata hiyo akishindwa katika kura za maoni.
Diwani wa Kata ya Mwanzange Mheshimiwa Rashid Jumbe |
Akizitaja
Kata ambazo tayari zimepata wagombea wake ni kata ya ngamiani Kaskazini-Mheshimiwa
Akida,Kata ya Ngamiani Kati-Habibu Nabahani Mpa,Kata ya ngamiani Kusini-Musa
Bakari Mbaruku,Kata ya Mwanzange-Rashid Jumbe,Kata ya Marungu-Mheshimiwa
Bori,Kata ya Tongoni-Nasoro Mohamed,Kata ya Kirare-Mheshimiwa Mnangwa,Kata ya Tangasisi-Mohamed
Haniu Pen,Kata ya Kiomoni-Mheshimiwa Mwakuro Bakari,Kata ya Mabawa-Mheshimiwa
Mwasabu,Kata ya Chongoleani-Mheshimiwa Akida Mswahili Njama,Kata ya
Mzizima-Kijana Muft,Kata ya Mabokweni-Jumaa Mbega,Kata ya Makorora-Omari Salehe
Mzee.
Mheshimiwa
Jumbe akizungumzia kuhusu suala zima la UKAWA kuachiana nafasi za ugombea
katika nafasi mbali mbali kutokana na
nafasi zote za hapa Tanga kuonekana kama CUF wamezishikilia sana,amesema
kuwa UKAWA ipo ila kwa sasa wanasubiri katika nafasi ile ya
kumpata mgombea wa Urais ikamilike ili wakae katika meza moja wafanye
mazungumzo lakini watakaa kwa vigezo na nguvu ya chama itatumika kutokana na
sehemu husika ili kupata maridhiano.
Mheshimiwa
Rashid Jumbe amelitolea pia ufafanuzi kuhusu suala zima la ongezeko la majimbo
kwa upande wake amesema kuwa hakubaliani nalo labda jimbo la Handeni anakubaliana nalo
lakini hayupo tayari kuunga mkono ongezeko la majimbo ya uchaguzi kwani kufanya hivyo ni kutumia viabaya pesa za umma.
No comments:
Post a Comment