Home Traders

Home Traders

Tembelea TK FM Redio 88.5 Tanga

Wednesday, 15 July 2015

UKAWA ngoma mbichi bado sasa kumtangaza mgombea wao baad ya Siku 7

Umoja wa Katiba Ya Wananchi UKAWA unajipanga kikamilifu kumtangaza mgombea wake wa kiti chaUrais kwa shamra shamra  mgombea huyo ambaye Watanzania wengi wanamsubiri kwa hamu kubwa, akizungumza mbele ya waandishi wa habari katika hoteli ya Colosseum jijini Dar es salaam hapo jana Jumanne 14 Julai 2015, Mwenyekiti wa Chama Cha NCCR Mageuzi Mhe. James Mbatia, amesema ndani ya siku saba watakuwa tayari wameshamtangaza mgombea wao.

 Mbatia amesema kuwa  wameafikiana na vyama vyote vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA , kila mmoja kwenye chama chake kwa kufuata demokrasia amechaguliwa mgombea mmoja na kwa mardhiano ya hali ya tumepata mgombea mmoja ambae tunajipanga kumtangaza kwa mashamsham” alisema Mhe. Mbatia.

Swala lingine alilolizungumzia Mhe. Mbatia ni la uvumi ya kwamba CUF imejitoa UKAWA, akijibu swali hilo lililoulizwa na mwandishi wa habari, Mhe. Mbatia alisema kwamba taarifa hizo hazina ukweli wowote kwani ameongea na Profesa Lipumba na kauli yake ya mwisho amesema yeye yupo UKAWA, kwa hiyo taarifa zilizoenea kwamba CUF imejitoa UKAWA sio za kweli, ila Mhe. Lipumba alikuwa na majukumu ya kikazi ndo maana hakuwepo kwenye kikao hicho.

Kuhusiana na Mhe. Lowassa kuhamia UKAWA kama  taarifa  zilivyotapakaa kwenye mitandao, Mhe. Mbatia amesema huo ni uzushi tu, kwenye mitandao kila mmoja anaandika lake, mbona baada ya Mhe. Edward Lowassa kukatwa kugombea kiti cha Urais kupitia CCM habari zilienea kwenye mitandao kuwa amehamia ACT Wazalendo lakini taarifa hiyo haikuwa na ukweli wowote ni taarifa za mitandaoni tu.
Mhe. Mbatia akuzungumzia kwanini kikao kimekuwa kirefu hivyo,  alisema licha ya kuwa na mchakato mrefu wa kumpata mgombea wa Urais kupitia UKAWA katika uchaguzi wa Oktoba 2015, pia walikuwa wakizungumzia majimbo 26 mapya, vipi watagawana, huku kukiwa na mwezi mmoja tu kuanza kampeni,huku kukiwa na majimbo mapya ambayo hata hayaonyeshi mipaka ilipo,hivyo ili wakae na wataalam ili wajue nini cha kufanya,hii inaonyesha ni jinsi gani serikali isovyojali wananchi wake, kwa nchi masikini kama Tanzania kuongeza majimbo ni kujiongezea gharama tu.

No comments:

Post a Comment