Home Traders

Home Traders

Tembelea TK FM Redio 88.5 Tanga

Friday, 19 August 2016

Malinzi Amlilia Kelvin Haule

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amemtumia salamu za rambirambi Mwenyekiti wa Klabu ya Majimaji ya Songea, mkoani Ruvuma, Humphrey Millanzi kutokana na kifo cha mchezaji wa zamani wa timu hiyo, Kelvin Haule kilichotokea jana Agosti 18, 2016 kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma.


Rais Malinzi amemuelezea Haule kuwa alikuwa na mchango mkubwa katika mafanikio ya timku ya Majimaji ya Songea na Lipuli ya Iringa hivyo ameacha alama ya ucheshi, kujituma na uwajibikaji katika kufanikisha kazi zake katika timu ambazo alichezea.

Salamu za rambirambi za Rais wa TFF Malinzi pia zimekwenda kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiki na kuwataka kuwa na moyo wa subira wakati huu mgumu wa msiba wa Kelvin Haule.

Mwenyezi Mungu aipumzishe roho ya marehemu Kelvin Haule mahala pema peponi.

Bwana alitoa, Bwana alitoa, jina la Bwana lihimidiwe.

KUIONA SERENGETI BOYS, AFRIKA KUSINI SH 2,000, SH 5,000

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetangaza kiingilio cha Sh 2,000 kwa mzunguko na Sh 5,000 kwa jukwaa kuu wakati timu ya taifa ya Tanzania ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 itakapocheza na Amajimbos ya Afrika Kusini kwenye mchezo wa kuwania nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika  zitakazofanyika Madagascar, mwakani.

Mchezo huo utakaoanza saa 9.00 alasiri Jumapili Agosti 21, 2016 kwenye Uwanja wa Azam ulioko Chamazi – Mbagala, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam utachezeshwa na Mwamuzi Noiret Jim Bacari wa Comoro akisaidiwa na Mmadi Faissoil na Said Omar Chebli wakati mezani atakuwa Ali Mohamed Adelaid huku Kamishna wa mchezo huo atatoka Somalia ambaye anaitwa Amir Abdi Hassan.

Jumamosi Agosti 6, 2016, Serengeti ilitoka sare ya 1-1 na Afrika Kusini katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Dobsonville ulioko Soweto, Mji ulioko Kusini – Magharibi mwa jiji la Johannesburg, mabao yote yalipatikana kipindi cha pili yakiwa ni ya penalti kwa kila upande. Afrika Kusini ndio walioanza kupata penalti katika dakika 65 iliyofungwa na Luke Gareth kabla ya Ally Msengi kuisawazishia Serengeti Boys katika dakika ya 70.

Penalti ya Afrika Kusini ilitokana na mmoja wa mabeki wa Serengeti Boys kumfanyia madhambi Linamandla Mchilizeli wa Amajimbos ndani ya eneo la hatari wakati ile ya Serengeti Boys ilitoakana na beki Luke Donn wa Amajimbos kunawa mpira eneo la hatari. Mwamuzi wa mchezo huo alikuwa, William Koto kutoka Lesotho.

LIGI KUU BARA KESHO NI KESHO,VITA YA MASAU BWIRE NA TOBIAS KIFARU IMEREJEA TENA

Je kweli Simba  watahitaji kutumia mbinu na akili kushinda  katika mchezo wa kesho?Tusubiri tuone……


Pazia la Ligi Kuu Bara msimu mpya wa 2016/2017 litafunguliwa  kesho Jumamosi Agosti 20, timu 14 zitakuwa katika viwanja tofauti kusaka ushindi katika mechi zao za kwanza za msimu, mechi zote zitakuwa na ushindani mkubwa kwani kila timu haitaki kubaki nyuma, kila mmoja anahitaji kuanza kwa ushindi.

Simba vs Ndanda

Licha ya maandalizi mazuri waliyokuwa nayo Simba haitakuwa rahisi kwao kupata ushindi dhidi ya Ndanda kama wanavyodhani, Wekundu wa Msimbazi wanatarajiwa kupata upinzani mkubwa siku hiyo kutoka kwa Ndanda, timu hiyo kutoka Mtwara ni moja ya klabu ngumu Ligi Kuu  na wanacheza kwa ushirikiano na kujituma muda wote dimbani, kwa hakika patachimbika.

Simba inataka kurejesha heshima yake, na Ndanda wanataka kudhihirisha kuwa si wa kudharauliwa.

Mtibwa vs Ruvu Shooting

Achana na vita vya uwanjani, vita kubwa ipo baina ya wasemaji wa klabu hizo, ambao ni marafiki wakubwa, Mtibwa Sugar ambayo msemaji wake ni Thobias Kifaru na Ruvu Shooting ambayo inawakilishwa na Masau Bwire, wasemaji hawa ndio wanafanya mechi hii kuwa na mvuto hasa kutokana na maneno yao ya kejeli nje ya uwanja.Msimu uliopita Kifaru alimmisi sana swahiba wake masau na sasa vita vinaendelea.



Stand utd v/s mbao  fc

Timu ya mbao inaingia uwanjani ikiwa  imependa ligi kuu msimu huu huku ikicheza na timu ambayo imekubwa sana na migogoro ya kiuongozi huku kila  timu inahitaji  kushinda katika mchezo wa kesho lakini wengi wakiipa nafasi timu ya stand utd kutokana na uzoefu wa ligi hiyo.

Majimaji v/s tanzani prisons

Huu ni mchezo mwngine pia tukiushuhuda kesho  pale maji maji watakapowakaribisha  Tanzania prisons huku timu zote zikiwa na uzoefu na mikiki mikiki ya ligi kuu Tanzania bara.

Azam fc v/s African Lyon

Mchezo huu utachezwa usiku pale chamanzi badala ya saa kumi  jioni kutokana na kesho jumaosi kutakuwa na mazoezi ya timu ya afrika kusini chini ya umri wa miaka 17 kuutumia uwanja wa chamanzi kwa ajili ya kufanya mazoezi.

HATA HIVYO

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linaonya timu kuchezesha wachezaji wa kigeni kama hawana vibali vya kuishi, kufanya kazi na leseni inayomruhusu kucheza ligi husika kwa mujibu wa sheria za nchi na kanuni za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Vibali vya kuishi na kufanya kazi vinatolewa na Idara ya Uhamiaji Tanzania (Uhamiaji) wakati leseni ya kucheza inatolewa na TFF. Vilevile tumeziagiza klabu kulipia ada za ushiriki kwa kila timu; leseni za wachezaji, ada za wachezaji na ada za mikataba. Mchezaji hatapewa leseni ya kucheza kama uongozi wa timu hautakamilisha taratibu za malipo.

TFF linapenda kuzikumbusha timu zinazoshiriki Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwamba hatutatoa leseni ya mchezaji yeyote ambaye timu haikuleta mkataba wakati wa maombi ya usajili, hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 68 vipengele vya 1, 2, 3 na 8 ya Ligi Kuu ya Tanzania toleo la 2016/2017.

Kila timu inatakiwa kuleta nakala tatu za mkataba wa mchezaji, ili kamati ya katiba, sheria na hadhi za wachezaji iweze kupitia na TFF iweze kuidhinisha mikataba hiyo. Baada ya hapo timu na mchezaji, watakuja kuchukulia mikataba hiyo hapa TFF. 

TFF YAMPA TANO KESSY,SASA KUKIPIGA RASMI JANGWANI

Kamati ya Sheria na Haki za wachezaji imepisha usajili wa wachezaji wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara huku ikiwa imepitisha jina la Hassan Ramadhani ‘Kesi’ kuitumikia Young Africans kuanzia msimu huu 2016/17 baada ya kuona kuwa hana tatizo katika usajili badala yake madai ambayo pande husika zinaweza kudaiana wakati mchezaji anaendeleza kipaji chake.
Simba ilikuwa ikimtuhumu Kessy kuvunja mkataba kwa kuanza kuvaa jezi, kufanya mazoezi, kusafiri na kushiriki shughuli mbalimbali za mabingwa hao wa VPL msimu uliopita wakati muda wa mkataba wake na Wekundu hao wa Msimbazi haujafika kikomo.
Kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake, Richard Sinamtwa imepitia usajili wa timu zote na kujiridhisha kwamba suala la mchezaji Hassan Kessy limeegemea kwenye madai na si usajili ambako Simba ndiye mdai kwa kumtuhumu mchezaji huyo kuwa alianza kuitumikia Young Africans kabla ya kumaliza mkataba wake Simba SC. Mkataba wake ulifika mwisho, Juni 15, 2016.
Kama ni madai Simba inaweza kuendelea kumdai Kessy au Young Africans wakati mchezaji huyo anatumika uwanjani kwa mwajiri mpya. TFF inafuatilia na kuangalia haki ya Simba namna ya kupata haki yake baada ya kuwasilisha madai kuhusu kuvunja mkataba na mwajiri wake wa zamani.
Kanuni hazimzuii mchezaji kuendelea kucheza kwa hoja ya madai badala yake suala hilo linaweza kumalizwa wakati mashindano yanaendelea. Kamati inaendelea kupitia malalamiko na pingamizi za wachezaji wengine na inatarajiwa kutoa taarifa rasmi kuhusu wachezaji wote wakati wowote kuanzia sasa.

Sunday, 14 August 2016

TORABORA FC KUFANYA MKUTANO MKUU JUMAPILI

Timu ya Tora Bora Fc yenye maskani yake barabara ya kumi n atano 15 jijij hapa inatarajiwa kufanya m kutano wao mkuu wa wanachama na washabiki wa timu hiyo siku ya jumapili tarehe  21/8/2016.

Akizungumza na TK FM  REDIO katibu mkuu wa timu hiyo  KASETA BOTO KAMCHALA maarufu Boto Man amesema kuwa lengo kuu la mkutano huo ni  kuwatambulisha wanachama  uongozi wao na kuwakusanya wapenzi na wanachama kuwaelezea mustakabali wa timu pamoja na maandalizi ya timu yao.

Aidha Boto amesema kuwa mkutano huo utakuwa na ursa ya kutoa kadi kwa wanachama wapya watakaojiumga na timu hiyo ya TORA BORA FC.